NIDA KUANZA KAZALISHA VITAMBULISHO 180,000 KWA SIKU
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene amesema mitambo mipya ya uzalishaji wa vitambulisho vya taifa itaanza kufanya kazi hivi karibuni baada ya wataalamu kuwasili nchini na ambapo sasa NIDA itakuwa na uwezo wa kuzalisha vitambulisho 180,000 kwa siku.
Simbachawene amesema mitambo hiyo ilishafungwa muda mrefu ofisini za NIDA na ilipaswa iwe imenza kufanya kazi tangu mwezi Aprili, mwaka huu lakini kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Corona ilichelewa kuanza kufanya kazi kutokana na watalaamu wa mitambo hiyo kutoka Ujerumani kushindwa kuja nchini.
sponsored by
#AzamTVUpdates #AzamNews #MilardAyo #BrightSide.